The State of Membership and Contribution to ZIRPP – An Update

2 09 2009

Dear Friends and Colleagues,

Please be informed that, as of 01 September 2009, the following Zanzibaris have formally registered as members by duly filling in the application forms and paid up their annual subscription fees plus voluntary contributions to the Institute:

NAME AMOUNT PAID IN TSHS.

1. Mr. Muhammad Yussuf 400,000.00
2. Ms. Angelika Sepetu 13,500.00
3. Ms. Fatma Gharib Bilal 150.000.00
4. Mr. Abdulla Ghassani 100.000.00
5. Mr. Mohamed Khamis Baucha 100,000.00
6. Mr. Nassor Mugheiry 52,000.00
7. Ms. Mariam Mohammed Hamdani 50,000.00
8. Mr. Jumbe Said Ibrahim 50,000.00
9. Mr. Mbarouk Shaaban 50,000.00
10. Ms. Asha Abdulla 50,000.00
11 Mr. Ahmed Khamis 50,000.00
12. Mr. J. V. Karim 40,000.00
13. Mr. Farouk Karim 15,000.00
14. Mr. Shaaban Mgambo 15,000.00
15. Mr. Khamis Abdulla Ameir 15,000.00
16. Mr. Sheraly Champsi 13,500.00
17. Ms. Mwanaache Mohamed Haji 1,000.00
18, Ms. Zulekha Chully Ramadhan 1,000.00
19. Mr. Hafidh Ismail Omar 1,000.00
20. Mr. Nassor Ali Iddi 1,000.00
21. Mr. Abdulrahaman Muhammad Masoud 1,000.00
22. Ms. Alya Sened 1,000.00
23. Mr. Haji Machano Haji 13,500.00
24. Mrs. Maheba Juma Bakari 15,000.00
25. Dr. Mayasa Salum Ally 15,000.00
26. Mr. Bakar Juma Bakar 20,000.00
27. Mr. Bushiri Mahmoud Rajab 13,500.00
28. Mr. Abdulla Maulid 13,500.00
29. Mr. Narendra Gajjar 30,000.00
30. Mr. Mohammed Fakih Mohammed 50,000.00
31. Mr. Othman S. Khatib 20,000.00
32. Mr. Said Mmaka 13,500.00
33. Mr. Khamis Kombo Songoro 30,000.00
34. Mr. Abdillahi Yussuf 15,000.00
35. Mr. Marumbo Hussein Bakari 15,000.00
36. Mr. Mwinchande Sheha Khamis 13,500.00
37. Ms. Hindi Said Shindano 15,000.00
38. Ms. Salma Hamoud Said 15,000.00
39. Mr. Mohammed Khamid Hamad 15,000.00
40. Mr. Ally Saleh Abdullah 15,000.00
41. Mr. Farook Ahmed Elias 50,000.00
42. Ms. Kulthum Yussuf Himidi 20,000.00
43. Mr. Aboud Talib Aboud 14,000.00
44. Mr. Mkwale Adam Taib 14,000.00
45. Mr. Abbas Fadhil Abbas 14,000.00
46. Mr. Abdulla Muhiddin Jaha 15,000.00
47. Mr. Hamid Ramadhan Tiptip 15,000.00
48. Mr. John Doe 20,000.00
49. Mr. Hamza Zubeir Rijal 13,500.00
50. Ms. Mwantanga Ame 15,000.00
51. Prof. Ali Seif Mshimba 16,000.00
52. Mr. Juma Duni Haji 20,000.00
53. Mr. Ismail Jussa Ladhu 30,000.00

The following members have paid up their annual fees and voluntary contributions in US Dollars:

NAME AMOUNT PAID IN USD

1. Dr. Omar Juma Khatib 200.00
2. Dr. Mohamed Adam 150.00
3. Mr. Mohammed Saleh 145.00
4. Dr. Muhammad Juma 135.00
5. Ms.Talha Muhammad Yussuf 150.00
6. Dr. Hassan Omar Ali 154.00
7. Dr. Harith Ghassany 154.00
8. Amb. Ali A. Karume 140.00
9. Sheikh Abdulla Al-Harthy 100.00

I wish to take this opportunity to express, on behalf of the Institute, our sincere thanks and gratitude to all these men and women for filling in the application forms and paid up their annual contributions in full and on time. We are also grateful for those who made additional payments in the form of voluntary contributions to the Institute for their generosity. Indeed, this a vivid manifestation of their unflinching commitment to the work and ideals of the Institute for which we are highly appreciative.

Finally, we would like to take this opportunity to urge all those Zanzibaris (and non Zanzibaris alike) who have not yet filled in the application forms to do so as soon as possible. Your invaluable contributions to the Institute will be highly appreciated.

Thanking you in advance for your continued support and understanding.

Warm Regards,

Muhammad Yussuf
Interim Executive Director
Zanzibar Institute for Research and Public Policy
P.O. Box 416
Zanzibar
TANZANIA
Tel: 0777 707820 Cellular
Tel: 0242 233526 Office
Email: yussufm@gmail.com





Marekani yaonya raia wake kutoenda Zanzibar

2 09 2009

Na Claud Mshana

MAREKANI imetahadharisha raia wake kuepuka safari zote zisizo za lazima visiwani Zanzibar kutokana na hofu ya kuibuka kwa zinazohusiana na uchaguzi wakati visiwa hivyo vikiwa kwenye zoezi la kuandikisha wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
Tahadhari hiyo, ambayo inaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa uchumi wa visiwa hivyo unaotegemea utalii, imetolewa wakati Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ikiwa imesimamisha zoezi hilo la kuandikisha wananchi kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura baada ya kutokea vurugu zilizosababisha watu kadhaa kujeruhiwa kisiwani Pemba.

Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani iliyotolewa jana imesema kuwa zoezi la kuandikisha wapiga kura limesababisha machafuko na hivyo kuwataka Wamarekani kuwa makini wanapotaka kufanya safari kwenye visiwa hivyo.
“Wizara ya Mambo ya Nje inawatahadharisha raia wa Marekani uwezekano wa kuwepo vurugu zinazohusiana na uchaguzi kwa sababu Zanzibar inaanza kuandikisha wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kuwa Oktoba 2010,” inaeleza taarifa hiyo iliyotumwa kwenye tovuti ya wizara hiyo.

“Wizara (ya Mamo ya Nje) inashauri kwamba raia wa Marekani waepuke safari zisizo na umuhimu za kwenda kisiwa cha Pemba cha Zanzibar. Tahadhari hiyo ya safari itadumu hadi Desemba 20,2009.
“Tangu uandikishaji wapiga kura kisiwani Pemba uanze Julai 6, 2009, kumekuwepo na taarifa nyingi kuhusu kutetereka kwa amani. Chaguzi zilizopita Zanzibar zimekuwa na matukio ya vurugu wakati wa msimu wa kampeni na wakati wa uchaguzi, na hasa katika siku na wiki zinazofuata baada ya matokeo kutangazwa.

“Vikosi vya usalama vya serikali vimeongezwa kaskazini mwa kisiwa cha Pemba, hasa kwenye wilaya za Wete na Micheweni. Uandikishwaji wapiga kura kwenye kisiwa cha Pemba unatarajiwa kumalizika Desemba 14.

Uandikishaji wapiga kura kwenye kisiwa kikubwa cha Unguja (pia kinajulikana kama Zanzibar) unatarajiwa kuanza Septemba na unaweza kugubikwa na mvutano wa kisiasa.“

Taarifa hiyo imeongeza kuwa Wamarekani wanaosafiri kwenda Zanzibar katika kipindi hiki wanakumbushwa kuwa katika tahadhari kubwa ya usalama wakati wote na kuepuka mikutano ya kisiasa, maandamano na mikusanyiko ya aina yoyote ile
Taarifa hiyo imewataka Wamarekani kufuatilia matukio ya hali halisi kupitia vyombo vya habari.

Wizara hiyo pia imewashauri hata raia wa Marekani wanaosafiri wanaokuja Tanzania, kujiandikisha kwenye ubalozi wa nchi hiyo kw akupitia tovuti ya serikali ili wapewe taarifa kuhusu safari na usalama wakati wakiwa Tanzania na kwamba wale ambao hawana huduma ya internet waende moja kwa moja kwenye ofisi za ubalozi.

Hali ya kisiasa Zanzibar imekuwa tete tangu zoezi la uandikishaji wapiga kura lilipoanza baada ya wananchi kupinga sheria iliyowekwa kuwa wanaoandikishwa ni wale tu walio na vitambulisho vya ukaazi wa Zanzibar, wakisema kufanya hivyo ni kukiuka katiba ambayo inamtambua Mzanzibari wenye nyaraka nyingine kama vyeti vya kuzaliwa.

Ilifikia wakati wananchi wa Pemba waliamua kufanya vurugu kukwamisha zoezi hilo na walifanikiwa baada ya serikali kutangaza kusitisha uandikishwaji wapiga kura.

Chama kikuu cha upinzani visiwani humo, CUF, kimekuwa kikipinga utaratibu mzima wa uandikishwaji na kimetishia kukwamisha zoezi hilo kama serikali haitaondoa suala la kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi kama sifa kuu ya kuandikishwa kupiga kura.

CUF inadai kuwa hali ni mbaya kisiwani Pemba kutokana na ukweli kuwa katika eneo lenye watu 400 ni idadi ndogo sana ya watu kati ya 40 na 50 walioandikishwa kutokana na wengi kukataliwa kwa kukosa kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi.

Utalii umekuwa na mchango mkubwa kwenye uchumi wa Zanzibar, ukitoa takriban ajira 200,000 na malengo ya serikali ni kuhakikisha visiwa hivyo, ambavyo vina historia ya aina yake na vivutio vingi, vinakuwa kituo kikuu cha watalii duniani kote.

Naye Mkinga Mkinga anaripoti kuwa Serikali ya Mapinduzi (SMZ) imeishutumu Marekani kwa onyo ililolitoa kwa wananchi wake kuhusu kutotembelea kisiwa cha Pemba kwa madai ya kutokuwepo uhakika wa usalama.

Akizungumza na Mwananchi jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alisema Marekani watakuwa na agenda yao ambayo hawataki kuiweka wazi ili ulimwengu ufahamu.
“Marekani wanashangaza… na kitu ambacho hakiingii akilini hata kidogo kusema kwamba Pemba hakuna aman,” alisema Juma.

Aliongeza kusema: “Pemba kuko shwari sana; nashangaa kusikia hata hiyo ‘warning (onyo)’ yao inatokana na kitendo gani hasa kilichofanywa huko Pemba?”

Alisema kuwa anawakaribisha Pemba watu wa mataifa mbalimbali kuona jinsi hali ilivyo shwari na kwamba wananchi wanaendelea na shughuli zao kama kawaida na wala hakuna vurugu kama ambavyo imesemwa na Marekani katika taarifa yake.

“Huko Pemba kuna raia wengi wa kigeni ambao wanaendesha biashara zao, mbona nchi zao hazijalalamika kuwa kuna vurugu kama inavyodaiwa na Marekani?,” alihoji Juma.

Alisema Zanzibar haiwezi kukubali uongo unaoenezwa na Marekani hata kidogo.

Chanzo: Mwananchi





SMZ acheni kuishutumu Marekani jirekebisheni

2 09 2009

MAREKANI imewatahadharia raia wake kutopanga safari zisizo za lazima kwenda Pemba, baada ya kutokuwa na imani ya usalama katika eneo hilo wakati huu wa kuekea uchaguzi mkuu wa mwakani.
Pamoja na tahadhari hiyo, raia wa Marekani wanaofika nchini kwa ajili ya kwenda Zanzibar hutakiwa kufika kwanza katika ubalozi wa nchi hiyo uliopo Dar es Salaam ili kuhakikisha usalama wao wawapo nchini.
Hatua hiyo ya Marekani inashtua na inaitia doa si tu kwa Zanzibar, bali kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya jumuia ya kimaitaifa; hivyo kuleta athari kubwa za kiuchumi na kijamii. Ni dhahiri hatua hiyo, itaathiri kwa kiasi kikubwa utalii ambao ni moja ya nguzo za uchumi Zanzibar.
Si hivyo tu, katika mazingira ya aina hiyo, ni rahisi wageni kutoka Marekani na nchi nyingine duniani kuwa na mashaka na usalama wao wakija Tanzania; hivyo ni rahisi kubadili njia kwenda mahali pengine hadi watakaporidhika kuwa hali ni shwari.
Inasikitisha kuwa uamuzi huo mzito umeshafikiwa na taifa hilo, lakini kibaya zaidi ni pale juhudi za kurekebisha kasoro zinaposuasu, huku mamlaka husika zitoa kauli za kuilaumu Marekani badala ya kutafakri na kujisahihisha.
Mwezi uliopita mabalozi wa nchi za Jumuiya ya Ulaya (EU), Marekani na Canada walipo nchini walizitaka Serikali ya Muungano (SMT) na ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuhakikisha kuwa matatizo yailiyojitokeza wakati wa zoezi la marekebisho ya Daftari la Kudumu la Wapigakura na kusababishwa vurugu kisiwani Pemba yarekebishwe.
Badala ya kuona kuwa huo ni ushauri mzuri; kiongozi mmoja wa SMZ aliitunisha misuli Marekeni na kuwaonya mabalozi hao wasiingilie mambo ya ndani ya nchi na kutamba kwamba, Zanzibar ni nchi huru yenye katiba yake.
Cha kushangaza, kauli hizo zimerudia tena juzi baada ya taarifa ya Marekeni kuwatahadharisha raia wake kutoenda Pemba kama ambavyo Naibu Waziri wan chi, Ofisi wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alivyokaririwa na gazeti hili akiilamu nchi hiyo kuwa ina ajenda yake kwasababu Pemba hakuna tatizo lolote.
Ni vizuri SMZ wakawa wakweli kuhusu hali ya Pemba kwasababu kila mtu anajua vurugu zilitokea, ndiyo maana zoezi la uandishaji lilisimamishwa. Matukio kama hayo yanaashiria kuwa hali inaweza kwa mbaya hasa wakati kama huu.
Historia inaonyesha kuanzia 1995; wakati wa mchakato, uchaguzi na baada hapo kunakuwa na vurugu Zanzibar na hasa Pemba, zinazosababisha baadhi yao watu kujeruhiwa au kupoteza maisha yao. Tunaomba SMZ isiilamu Marekani bali ichukue hatua zinazostahili kufuta doa hilo.

Chanzo: Mwananchi